TANGAZO LA KUAHIRISHWA KWA USAILI WA TAMISEMI KADA YA PROJECT FINANCE AND ADMINISTRATION OFFICER II

       Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI anapenda kuwataarifu Waombaji Kazi waliokuwa wameitwa kwenye usaili kwa ajili ya nafasi ya Project Finance and Administration Officer II, kupitia tangazo lenye Ref.No.JA.9/259/01/4 la tarehe 15 Julai, 2021 kuwa usaili huo umeahirishwa mpaka hapo watakapotangaziwa tena/itakapotolewa taarifa nyingine

      Sekretarieti ya Ajira inawaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza kutokana na kuahirishwa kwa usaili huo.

Imetolewa na;

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Sekretarieti ya Ajira

19 Julai, 2021