TAARIFA KWA UMMA, TAARIFA YA KUHAMIA DODOMA KWA OFISI ZA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

 

                                                  TAARIFA KWA UMMA                                                                                     

Dar es Salaam, Desemba 5, 2020                

     TAARIFA YA KUHAMIA DODOMA KWA OFISI ZA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anapenda kuwafahamisha Watanzania na wadau wote kuwa makao makuu ya ofisi zake yamehamia Dodoma. Hivyo, kuanzia tarehe 15 Desemba, 2020 huduma mbalimbali kuhusu masuala ya uendeshaji wa mchakato wa ajira zitakuwa zinapatikana Dodoma katika majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) zilipo baadhi ya ofisi za Wizara mama (Utumishi) na eneo linalojulikana kwa jina la “Asha Rose Migiro Square”.

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nasi kupitia anwani zifuatazo;-

  1. Ofisi ya Rais

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

Majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na

Eneo la“Asha Rose Migiro Square”.

S.L.P. 2320 - Dodoma

Simu: +255 22 2153517- 0735- 398259 0736-005511

Katibu@ajira.go.tz au gcu@ajira.go.tz au malalamiko@ajira.go.tz  

www.ajira.go.tz

 

  1. Ofisi ya Rais

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma

Ghorofa ya tatu

Jengo la Sheria House- Mazizini

Au ilipo ofisi ya Kamisheni ya Wafu na Mali Amana (MAMBO MSIGE)

S.L.P. 1272 - Zanzibar.

           Barua pepe: Zanzibaroffice@ajira.go.tz

 

Tunaomba radhi wadau wetu kwa usumbufu wowote utakaoweza kujitokeza.

Imetolewa na;-                                      

Riziki V. Abraham

                                            Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.