Wasailiwa wote waliopangiwa kufanya usaili katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) – Dar es Salaam kwa tarehe 01 na 04 Novemba, 2024 mnajulishwa kuwa usaili wa Kuandika kwa njia ya mtandao ( online) kwa tarehe 01/11/2024 na tarehe 04/11/2024 utafanyika katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph (SJUIT) kilichopo Mbezi, Jijini Dar es salaam badala ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha ( IFM ) kama ilivyoonekana katika akaunti zenu hapo awali.